Stori : Gladness Mallya na Hamida Hassan
OOOH! Zikiwa zimepita siku chache tangu
staa wa filamu Bongo , Wastara Juma
kunusurika kifo baada ya kudaiwa kunywa
sumu na baadaye kupata ajali , anadaiwa
kusumbuliwa na roho wa kifo .
Wastara Juma .
Kupitia ukurasa wake katika Mtandao wa
Kijamii wa Instagram, Wastara aliweka
picha za wasanii mbalimbali huku
akimwelezea kila mmoja alivyo na mwishoni
mwa maelezo hayo alimalizia kwa kusema
kuwa ameamua kusema kabla hajafa kwani
kifo hakiko mbali .
00Baadhi ya mastaa aliowaelezea ni
Tamrina Poshi ‘ Amanda’, Denis Swea ‘Dino ’ ,
Jacob Steven ‘JB ’, Steven Mengere ‘ Steve
Nyerere ’, Halima Yahya ‘ Davina’, Riyama
Ally, Salma Jabu ‘ Nisha’.
Wengine ni Cloud , Lamata , Bondi , Msafiri
Kondo na wengineo ambapo baada ya
kumuelezea kila mmoja , chini alikuwa
akiandika ujumbe huu:
“Sababu ya kufanya hivi, sisi ni binadamu
na kifo hakiko mbali , naweza nikafa kabla
sijasema lolote kwa watu wangu .”
WASTARA ANASEMAJE ?
“Niliandika maneno hayo ili wasanii wote
waliowahi kunitendea wema wajue kwamba
wao ni watu muhimu sana katika maisha
yangu , wapo wengi lakini sikuweza
kuwashukuru wote kwa sababu wakati
naandika hivyo nilikuwa kwenye hali mbaya
sana.
“Unajua siku moja nitakufa maana kifo
kiko karibu sana hivyo watakumbuka
maneno yangu hayo niliyoandika ya
kuwashukuru, ” alisema Wastara .
Baada ya kuwaelezea kwa kuwaandikia
waraka huo, mashabiki mbalimbali waliopo
kwenye mtandao huo walionekana
kusikitishwa na maneno hayo na kujikuta
wakimuuliza maswali yasiyokuwa na majibu
kwa wakati huo huku wengine wakidai kuwa
Wastara anasumbuliwa na roho wa kifo .
Monday, March 3, 2014
WASTARA ASUMBULIWA NA ROHO YA KIFO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment