Mesut Ozil akiifungia Arsenal bao la
kuongoza katika dakika ya 80 ya mchezo .
Ozil akishangilia na wachezaji wenzake
baada ya kufunga bao .
Gerard Deulofeu wa Everton ( kushoto)
akishangilia bao la kusawazisha dakika ya
81 ya mchezo .
Beki wa Arsenal Laurent Koscielny ( kushoto)
akijaribu kumzuia Steven Pienaar wa Everton
wakati wa mchezo huo.
Timu ya Arsenal imeshikwa baada ya kutoka
sare ya 1- 1 na Everton katika mechi ya Ligi
Kuu England iliyopigwa Uwanja wa Emirates
jijini London , Uingereza hivi punde.
Bao la kuongoza la Arsenal limewekwa
kimiani na Mesut Ozil dakika ya 80 kabla ya
Gerard Deulofeu kusawazisha bao hilo dakika
ya 84 na kufanya matokeo kuwa 1- 1.
Mpaka mwisho wa mchezo Arsenal 1 na
Everton 1. Kwa matokeo hayo bado Arsenal
wanaongoza ligi hiyo wakiwa na pointi 35
wakati Everton wapo nafasi ya tano wakiwa
na pointi 28.
Sunday, December 8, 2013
ARSENAL YASHIKWA EPL, YALAZIMISHWA SARE YA 1- 1 NA EVERTON
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment