Monday, March 3, 2014

NISHA AWA KITUKO KWA YATIMA


STAA wa filamu Bongo, Salma Jabu ‘ Nisha’
hivi karibuni alijikuta akigeuka kituko kwa
watoto yatima kutokana na mavazi ya
‘kihasara ’ aliyokuwa amevaa na kulazimika
kujistiri na mtandio kiunoni .
Salma Jabu ‘Nisha’ .
Nisha akiwa na timu yake (Team Nisha),
walikwenda kutoa msaada katika Kituo cha
Mwana Orphans Centre kilichopo Vingunguti ,
jijini Dar na walipofika walijishangaa kwa
kuwa watoto hao walikuwa wamevaa mavazi
ya heshima .
“Mh ! Imebidi nijistiri kidogo na mtandio
lakini kimsingi nimeguswa na watoto hawa
kwa sababu na mimi ni yatima na haya
maisha nimeyapitia hivyo kila mwisho wa
mwezi tutakuwa tukitembelea kituo hiki na
kuwaletea mahitaji muhimu , ” alisema Nisha.
Nisha na wenzake walitoa misaada ya vifaa
mbalimbali vikiwemo sabuni, vyakula na
vinywaji huku mmoja wao aliyekuwa na
‘bethdei ’ akikata keki na kula na watoto
hao.
Load Previous Comments

No comments:

Post a Comment

.