Monday, March 3, 2014

REHEMA FABIAN LAIVU


KhAA! Mshiriki wa Shindano la Miss Kiswahili
mwaka 2009 ambaye kwa sasa yuko nchini
China akijitafutia maisha, Rehema Fabian
amenaswa laivu akiwa kimahaba na kibabu
cha kizungu .
Miss Kiswahili mwaka 2009, Rehema Fabian ,
akiwa kimahaba na kibabu cha kizungu .
Akizungumza na Ijumaa Wikienda kwa njia
ya simu , mnyetishaji wetu ambaye naye
yuko nchini humo alisema kuwa kwa sasa
mrembo huyo anajiachia na babu huyo
ambaye kwa kumwangalia harakaharaka
anaweza kuwa sawa na mjukuu wake .
Rehema Fabian .
“Unajua mapenzi ya wazee ni mazuri sana ,
kwanza wanajua kubembeleza , isitoshe
hawakupi msongo wa mawazo mara kwa
mara kama yalivyo mapenzi ya vijana na
ndiyo maana Rehema akaona bora ajiachie
na kibabu , ” alisema mtonyaji huyo .
Rehema Fabian .
Baada ya kupata ‘ infomesheni ’ hizo ,
Ijumaa Wikienda lilimtafuta Rehema ili
kujiridhisha kuhusiana na stori hiyo ambapo
kwa upande wake alianza kucheka kisha
kudai aachwe ale ujana.
“Ahaha! Mshaanza mambo yenu , niacheni
jamani nile ujana, ” alisema Rehema .

No comments:

Post a Comment

.