Na Nicodemus Jonas
KIUNGO wa zamani wa maafande wa JKT
Oljoro, Yassin Juma Majota, amepata ulaji
katika Klabu ya Ajax Cape Town ya Afrika
Kusini ‘ Sauz ’ , baada ya kupewa nafasi ya
kufanya nayo mazoezi kwa kipindi cha miezi
miwili, kabla ya kusainishwa moja kwa moja .
Majota, 19 , aliyewahi kuitwa katika kikosi cha
timu ya taifa ya vijana , hadi anapata dili hilo,
alikuwa akiichezea Kinondoni FC baada ya
mkataba wake na Oljoro kumalizika msimu
uliopita .
Akizungumza na Championi Jumatatu,
Meneja wa Kinondoni FC, Saleh Alawi,
ambaye ndiye alimpeleka Sauz , alisema
mchezaji huyo kwa sasa ana wiki mbili tangu
aanze mazoezi na amekuwa akiendelea
vyema .
“Ana wiki mbili na anaendelea na mazoezi na
timu hiyo , sema tatizo bado hajapona vizuri
goti lake , hivyo anapewa mazoezi ambayo si
magumu zaidi , ikizingatiwa bado ni mdogo .
“Kuna matumaini akafuzu, maana baadhi yao
wanamjua uwezo wake, ndiyo maana
haikuwa kazi kuwashawishi . Tumuombee
apone kabisa goti na kusubiri
Sunday, December 8, 2013
Mchezaji Oljoro aula Sauz
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment