Kocha wa timu za vijana , Jacob Michelsen .
SHIRIKISHO la Soka Tanzania ( TFF ) ,
limeweka wazi kuwa halitamuongezea ajira
kocha wa timu za vijana , Jacob Michelsen
raia wa Denmark .
Uamuzi huo , umetangazwa leo na Rais wa
TFF , Jamal Malinzi, ambapo amesema
shirikisho lake limeona hakuna sababu ya
kumuongezea mkataba kocha huyo, ambao
unamalizika Desemba 15, mwaka huu.
Malinzi, amesema mara baada ya mkataba
huo wa Michelsen kumalizika , TFF itamsaka
mrithi wake, ambapo sasa Mtanzania
atachukua nafasi ya Mdenish huyo, ukiwa ni
mkakati maalum wa kuwapa wazawa nafasi.
“Tumeona hakuna haja ya kumuongezea
mkataba Jacob ( Michelsen ) , mkataba wake
wa sasa unafikia tamati Desemba 15, mwaka
huu na utakapomalizika ataondoka mara
moja na tayari tumeshamjulisha mapema juu
ya uamuzi huo , ” alisema Malinzi.
“Tumekubaliana kama TFF , kwamba mara
baada ya Jacob kuondoka nafasi yake
atafutwe kocha wa Kitanzania, mwenye
uwezo ili azibe nafasi yake , hii ni katika
kuwapa nafasi wazawa wenye uwezo wa
kufanya majukumu haya, tunajua kuwa watu
makini wapo.
Wednesday, December 4, 2013
TFF YAMNYIMA MKATABA MPYA MZUNGU WA KUWAPIKA VIJANA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment